Exodus 17:1-3

Maji Kutoka Kwenye Mwamba

(Hesabu 20:1-13)

1 aJumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Bwana alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa. 2 bKwa hiyo wakagombana na Musa wakisema, “Tupe maji ya kunywa.”

Musa akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Bwana?”

3 cLakini watu walikuwa na kiu huko, wakanung’unika dhidi ya Musa, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”

Copyright information for SwhKC